Yanga wamehuisha tena mpango wao wa kumsajili winga wa kimataifa wa Angola, Gelson Dala, kuelekea dirisha kubwa la usajili linalotarajiwa kufunguliwa mwezi ujao.
Katika dirisha dogo la usajili lililopita, Yanga ilifanya juhudi kubwa kumleta Dala kutoka klabu ya Qatar ya Al Wakrah SC, lakini mpango huo haukufanikiwa baada ya changamoto za uhamisho wake.





