International,Normal News,World Cup 2026, Canada, USA, Local

Kombe la Dunia 2026; Canada yapata pointi ya kwanza, Marekani yatoa onyo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Jun 2026
Kombe la Dunia 2026; Canada yapata pointi ya kwanza, Marekani yatoa onyo

Kombe la Dunia 2026 limeanza kwa shamrashamra kubwa huku mataifa mbalimbali yakianza safari ya kusaka ubingwa wa dunia. Mechi mbili zimeshuhudiwa usiku wa Ijumaa na Alfajiri ya Jumamosi katika makundi B na D.

Timu mwenyeji Canada ilianza kampeni yake kwa sare ya mabao 1-1 dhidi ya Bosnia na Herzegovina katika mechi iliyopigwa Toronto.

Bosnia walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Jovo Lukic kabla ya mshambuliaji Cyle Larin kuisawazishia Canada muda mfupi baada ya kuingia uwanjani kama mchezaji wa akiba.

Matokeo hayo yameiwezesha Canada kupata pointi yake ya kwanza kabisa katika historia ya ushiriki wao wa Kombe la Dunia la wanaume.

Kwa sasa, mechi nyingine ya kundi B kati ya Qatar na Switzerland itachezwa leo tarehe 13 Juni 2026.Β 

Msimamo wa Awali Kundi B

  • Canada – Pointi 1

  • Bosnia na Herzegovina – Pointi 1

  • Qatar – 

  • Switzerland – 

Kundi D: Marekani Yatoa Onyo kwa Wapinzani

Kundi D limeanza kwa kishindo baada ya Marekani kuifunga Paraguay mabao 4-1 katika mchezo wa ufunguzi wa kundi hilo. Folarin Balogun alikuwa nyota wa mchezo huo kwa kufunga mabao mawili, huku Gio Reyna akiongeza bao jingine na Paraguay kujikuta ikizidiwa katika maeneo mengi ya uwanja. Ushindi huo umeifanya Marekani kuongoza kundi mapema na kuonyesha dhamira ya kufanya vizuri mbele ya mashabiki wake wa nyumbani.

Msimamo wa Awali Kundi D

  • Marekani – Pointi 3

  • Paraguay – Pointi 0

  • Australia – 

  • Uturuki – 

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’