Local,Normal News,Ligi Kuu, Yanga, Mashujaa, Mbeya, Mtibwa

Yanga yaichapa Mashujaa Fc 2-0, yajiimarisha kileleni

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Jun 2026
Yanga yaichapa Mashujaa Fc 2-0, yajiimarisha kileleni

Yanga SC waliendelea kuthibitisha ubora wao kwenye ligi kuu baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo uliopigwa mkoani Kigoma, matokeo ambayo yamewapa nafasi nzuri zaidi kileleni mwa msimamo wa NBC Premier League.

Bao la kwanza la Yanga SC lilipatikana dakika ya 28 kupitia kiungo Mudathir Yahya, aliyefunga kwa shuti kali nje ya eneo la hatari baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Prince Dube.

Kipindi cha kwanza kilishuhudia Yanga wakitengeneza nafasi zaidi, lakini Maxi Nzengeli na Dube walikosa kutumia nafasi muhimu zilizoweza kuipa timu yao uongozi mkubwa mapema.

Kipindi cha pili, Yanga walionekana kupunguza kasi na kuwapa nafasi Mashujaa FC kutawala sehemu ya mchezo, hali iliyofanya mchezo kuwa na ushindani zaidi huku wenyeji wakijaribu kusaka bao la kusawazisha. Hata hivyo, ulinzi wa Yanga uliendelea kuwa imara na kuzuia mashambulizi mengi ya wapinzani wao.

Mchezo ulipofika dakika za mwisho, Yanga waliongeza bao la pili kupitia nahodha wao Bakari Mwamnyeto, aliyemaliza kwa ustadi baada walinzi wa Mashujaa Fc kushindwa kushindwa kuondoa hatari langoni.

Ushindi huo unaifanya Yanga SC kujiimarisha kileleni mwa ligi wakiwa na tofauti ya pointi tano dhidi ya wapinzani wao wa jadi Simba SC bada ya kufikisha alama 63.

Simba wanatarajiwa kucheza dhidi ya Pamba Jiji FC katika mchezo utakaopigwa siku ya Jumapili.

Katika mchezo mwingine wa mapema, Mbeya City FC waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar FC, matokeo ambayo yanaendelea kuwapa matumaini ya kupambana kuhakikisha wanabaki katika ligi kuu msimu ujao.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
48m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’