Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th June 2026


Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Juni 16, 2026 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatazo;

Ligi Kuu ya NBC

Mechi Namba 203: Mbeya City FC 1-0 Mtibwa Sugar

  • Klabu ya Mtibwa Sugar imetozwa faini ya Sh. 5,000,000 (milioni tano) kwa kosa la wachezaji na baadhi ya viongozi wa benchi la ufundi kuonekana wakifanya kitendo kinachoashiria imani za kishirikina kuelekea mchezo tajwa hapo juu.

  • Wachezaji hao na baadhi ya viongozi wa benchi la ufundi walijikusanya katikati ya uwanja na kuweka duara kuashiria kuomba dua lakini mmoja kati ya viongozi alionekana akichimbia vitu chini.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

  • Mwamuzi wa kati mchezo tajwa hapo juu, Liston Hiari kutoka Dar es Salaam ameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kwa mizunguko mitano (5) kwa kosa la kuonesha mapungufu ya kiuchezeshaji yaliyotokana na kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa miguu.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42:1(1.8) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Waamuzi.

Mechi Namba 205: Mashujaa FC 0-2 Young Africans SC

  • Shabiki wa klabu ya Young Africans aliyetambulika kwa jina la Said Selemani Ally amefungiwa kuingia uwanjani kwa kipindi cha miezi 12, kwa kosa la kuingia kwenye eneo la kuchezea siku moja kabla ya mchezo baada ya Young Africans kumaliza mazoezi yao ya mwisho na kumwaga vitu vyenye asili ya kimiminika na udongo kutokea goli la kusini kuelekea katikati ya uwanja kitendo kilichotafsiriwa kama imani za kishirikina.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 47:2 ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti kwa klabu.

Mechi Namba 205: Simba SC 2-1 Pamba Jiji FC

  • Mwamuzi wa kati Hance Mabena kutoka Tanga na Mwamuzi msaidizi namba moja (1) Frank Komba wa mchezo tajwa hapo juu, wameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kwa mizunguko mitano (5) kwa makosa la kuonesha mapungufu ya kiuchezeshaji yaliyotokana na kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa miguu.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42:1(1.8) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Waamuzi.

  • Klabu ya Simba imetozwa faini ya Sh. Milioni kumi (10,000,000) kwa kosa la mashabiki wake kumwagia maji mwamuzi msaidizi namba moja (1) wakipinga maamuzi ya mwamuzi huyo mara baada ya kunyoosha kibendera kuashiria mchezaji wa Simba kuotea.

  • Hili ni kosa la kujirudia kwa mashabiki wa klabu ya Simba ndani ya msimu huu wa 2025/2026, wakitenda kosa mfanano wa hilo katika michezo mitatu tofauti na kusababisha klabu kuadhibiwa.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

  • Klabu ya Pamba Jiji imetozwa faini ya Sh. Laki tano (500,000) kwa kosa la wachezaji wake sita (6) kuonyeshwa kadi za njano.

  • Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 47:10 kuhusu udhibiti kwa klabu.


  

More Stories

Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Today, READ MORE β†’
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Sowah kurejea Singida BS?
Sowah kurejea Singida BS?
Today, READ MORE β†’
Mubiru atua Azam Fc
Mubiru atua Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Today, READ MORE β†’
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Singida BS 5-0 Dodoma Jiji, Ligi Kuu
Singida BS 5-0 Dodoma Jiji, Ligi Kuu
Today, READ MORE β†’