International,Normal News,World Cup, Canada, Qatar, Local

Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026

Joel JJ By Joel JJ
19 Jun 2026
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026

Canada imeandika historia katika Kombe la Dunia 2026 baada ya kuibamiza Qatar mabao 6-0 katika mechi ya Kundi B iliyochezwa mjini Vancouver. Ushindi huo ni wa kwanza kabisa kwa Canada katika historia ya michuano ya Kombe la Dunia kwa wanaume.

Nyota wa Canada, Jonathan David, alikuwa gumzo la usiku huo baada ya kufunga mabao matatu (hat-trick) na kuiongoza timu yake kupata ushindi mkubwa wa kihistoria. Mabao mengine yalifungwa na Cyle Larin pamoja na Nathan Saliba huku Qatar pia ikijifunga bao moja.

Mchezo huo uligeuka kuwa mgumu zaidi kwa Qatar baada ya wachezaji wake wawili kuonyeshwa kadi nyekundu, hali iliyowapa Canada nafasi ya kutawala mchezo kuanzia kipindi cha kwanza hadi mwisho. Ushindi huo umeifanya Canada kupanda kileleni mwa Kundi B na kuongeza matumaini ya kutinga hatua ya mtoano.

Hata hivyo, furaha ya Canada iligubikwa na majeraha mabaya ya kiungo Ismaël Koné aliyelazimika kutolewa nje kwa machela baada ya kuumia vibaya mguuni. Tukio hilo lilisababisha taharuki kubwa uwanjani na hata kuzua mvutano kati ya wachezaji wa timu zote mbili baada ya mechi.

Mbali na ushindi wa Canada dhidi ya Qatar, michezo mingine imetoa matokeo yafuatayo:

  • Czechia 1-1 South Africa

  • Switzerland 4-1 Bosnia and Herzegovina

  • Mexico 1-0 South Korea

Matokeo hayo yameifanya Mexico kujiimarisha katika Kundi A ikiongoza kundi huku Switzerland nayo ikituma salamu kali kwa wapinzani wake katika Kundi B.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →