Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th June 2026


Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026

Canada imeandika historia katika Kombe la Dunia 2026 baada ya kuibamiza Qatar mabao 6-0 katika mechi ya Kundi B iliyochezwa mjini Vancouver. Ushindi huo ni wa kwanza kabisa kwa Canada katika historia ya michuano ya Kombe la Dunia kwa wanaume.

Nyota wa Canada, Jonathan David, alikuwa gumzo la usiku huo baada ya kufunga mabao matatu (hat-trick) na kuiongoza timu yake kupata ushindi mkubwa wa kihistoria. Mabao mengine yalifungwa na Cyle Larin pamoja na Nathan Saliba huku Qatar pia ikijifunga bao moja.

Mchezo huo uligeuka kuwa mgumu zaidi kwa Qatar baada ya wachezaji wake wawili kuonyeshwa kadi nyekundu, hali iliyowapa Canada nafasi ya kutawala mchezo kuanzia kipindi cha kwanza hadi mwisho. Ushindi huo umeifanya Canada kupanda kileleni mwa Kundi B na kuongeza matumaini ya kutinga hatua ya mtoano.

Hata hivyo, furaha ya Canada iligubikwa na majeraha mabaya ya kiungo IsmaΓ«l KonΓ© aliyelazimika kutolewa nje kwa machela baada ya kuumia vibaya mguuni. Tukio hilo lilisababisha taharuki kubwa uwanjani na hata kuzua mvutano kati ya wachezaji wa timu zote mbili baada ya mechi.

Mbali na ushindi wa Canada dhidi ya Qatar, michezo mingine imetoa matokeo yafuatayo:

  • Czechia 1-1 South Africa

  • Switzerland 4-1 Bosnia and Herzegovina

  • Mexico 1-0 South Korea

Matokeo hayo yameifanya Mexico kujiimarisha katika Kundi A ikiongoza kundi huku Switzerland nayo ikituma salamu kali kwa wapinzani wake katika Kundi B.


  

More Stories

Himid aongeza mwaka Azam Fc
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Today, READ MORE β†’
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Today, READ MORE β†’
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Today, READ MORE β†’
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Today, READ MORE β†’
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Today, READ MORE β†’
Pamba Jiji 4-0 Mtibwa Sugar, Ligi Kuu
Pamba Jiji 4-0 Mtibwa Sugar, Ligi Kuu
Today, READ MORE β†’
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Today, READ MORE β†’
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Yesterday, READ MORE β†’