Local,Normal News,CRDB Cup, Simba, Coastal

Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup

Joel JJ By Joel JJ
19 Jun 2026
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup

Makocha wa timu za Simba SC na Coastal Union wamezungumza kuelekea mchezo wa nusu fainali ya Kombe la CRDB utakaopigwa Jumamosi, Juni 20 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, mkoani Arusha, huku kila upande ukionesha kujiamini na maandalizi makini.

SIMBA YAAHIDI MAPAMBANO MAKALI NUSU FAINALI

Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema kikosi chake kipo tayari kwa mtihani huo mgumu dhidi ya Coastal Union, akisisitiza kuwa wamejipanga kuhakikisha wanatinga hatua ya fainali ya mashindano hayo ya taifa.

Barker alisema Simba inatambua ubora wa mpinzani wao, lakini maandalizi yao yamejikita katika kuhakikisha wanapata matokeo chanya.

“Tumejiandaa vyema na tupo tayari kwa mchezo huu wa nusu fainali Kombe la CRDB. Tunatambua ubora na ugumu wa Coastal Union. Mara ya mwisho tulipokutana nao Mkwakwani tulilazimika kutoka nyuma kupata ushindi,” alisema Barker.

Aliongeza kuwa kikosi chake kiko tayari kuonesha kiwango bora zaidi ili kufanikisha lengo la kufika fainali.

COASTAL UNION: TUNAHESHIMU SIMBA, LAKINI TUNAPAMBANA

Kwa upande mwingine, Kocha Mkuu wa Coastal Union, Fikiri Elias, amesema mchezo huo ni wa mtoano na si wa ligi, hivyo kila kitu kinaweza kutokea uwanjani.

Amesema timu yake imejipanga kimkakati na inajua ugumu wa mchezo huo, lakini inalenga kufanya vizuri na kufuzu fainali.

“Tunakwenda kushiriki mchezo wa mtoano na si ligi kuu, lazima mmoja apite kwenda fainali. Tumejipanga vizuri kimbinu, ingawa tunajua mchezo utakuwa mgumu sana,” alisema Elias.

Ameongeza kuwa historia ya mechi zilizopita dhidi ya Simba imekuwa fundisho kwao, na sasa wamejipanga kuonesha tofauti uwanjani.

“Historia ipo ili tujifunze, tumejifunza kwenye michezo iliyopita tuliyocheza dhidi ya Simba, kesho ndio mtaona tulichojifunza,” alisisitiza.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →