Local,Transfer News,Tetesi, Simba

Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Jun 2026
Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba

Klabu ya Simba SC imefikia makubaliano ya pande mbili na kiungo mshambuliaji Joshua Mutale maarufu kama Budo ya kuvunja mkataba wake, hatua inayomfanya nyota huyo kuwa mchezaji huru kuanzia sasa.

Taarifa zinaeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Mutale kumaliza kipindi chake cha mkopo katika klabu ya Al Adalah FC ya Saudi Arabia, huku timu hiyo ikiiarifu Simba kuwa haina mpango wa kumnunua moja kwa moja.

Mutale alikuwa bado amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na Simba, lakini kutokana na makubaliano hayo mapya, pande zote zimeamua kuhitimisha ushirikiano wao mapema na kumpa nafasi mchezaji huyo kuanza safari mpya ya soka akiwa huru kuchagua hatma yake.

Kiungo huyo alitua Simba SC kwa matarajio makubwa kutokana na kiwango alichokuwa amekionyesha kabla ya kusajiliwa, lakini alishindwa kuonesha makali yaliyotarajiwa ndani ya kikosi hicho katika kipindi chake cha kuitumikia klabu hiyo.

Baada ya kipindi chake cha mkopo kumalizika nchini Saudi Arabia, Mutale sasa anatajwa kurejea katika mazingira aliyoyazoea baada ya kuhusishwa na klabu yake ya zamani ya Power Dynamos, timu ambayo Simba ilimsajili kutoka huko misimu miwili iliyopita.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’