Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th June 2026


Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba

Klabu ya Simba SC imefikia makubaliano ya pande mbili na kiungo mshambuliaji Joshua Mutale maarufu kama Budo ya kuvunja mkataba wake, hatua inayomfanya nyota huyo kuwa mchezaji huru kuanzia sasa.

Taarifa zinaeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Mutale kumaliza kipindi chake cha mkopo katika klabu ya Al Adalah FC ya Saudi Arabia, huku timu hiyo ikiiarifu Simba kuwa haina mpango wa kumnunua moja kwa moja.

Mutale alikuwa bado amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na Simba, lakini kutokana na makubaliano hayo mapya, pande zote zimeamua kuhitimisha ushirikiano wao mapema na kumpa nafasi mchezaji huyo kuanza safari mpya ya soka akiwa huru kuchagua hatma yake.

Kiungo huyo alitua Simba SC kwa matarajio makubwa kutokana na kiwango alichokuwa amekionyesha kabla ya kusajiliwa, lakini alishindwa kuonesha makali yaliyotarajiwa ndani ya kikosi hicho katika kipindi chake cha kuitumikia klabu hiyo.

Baada ya kipindi chake cha mkopo kumalizika nchini Saudi Arabia, Mutale sasa anatajwa kurejea katika mazingira aliyoyazoea baada ya kuhusishwa na klabu yake ya zamani ya Power Dynamos, timu ambayo Simba ilimsajili kutoka huko misimu miwili iliyopita.


  

More Stories

Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Today, READ MORE β†’
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Today, READ MORE β†’
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Today, READ MORE β†’
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Today, READ MORE β†’
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Today, READ MORE β†’
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Today, READ MORE β†’
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Today, READ MORE β†’