Local,Normal News,CRDB Cup, Simba, Coastal

Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Jun 2026
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup

Mnyama Simba SC ameendelea kuonyesha ubabe wake baada ya kuichakaza Coastal Union kwa mabao 4-0 katika mchezo wa nusu fainali ya CRDB Bank Cup uliopigwa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, mkoani Arusha.

Ushindi huo umempa Simba tiketi ya moja kwa moja kwenda fainali, akiwaonyesha wapinzani wake kiwango cha juu cha soka la ushindani.

Simba yatakata utepe mapema

Kuanzia dakika za awali, Simba ilionekana kumiliki mchezo kwa asilimia kubwa, ikitengeneza mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Coastal Union. Presha hiyo ilizaa matunda dakika ya 19 kupitia kwa Libasse Gueye, ambaye alifunga bao la kwanza baada ya kuwatoka walinzi wa Coastal Union upande wa winga ya kulia kwa ustadi mkubwa.

Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kuendeleza ubabe wake. Dakika ya 55, shambulizi la Gueye lilisababisha bao la pili baada ya shuti lake kuokolewa na kipa Wilbroad Maseke wa Coastal Union, na mpira kumkuta Nickson Kibabage ambaye hakukosea kuiandikia Simba bao la pili.

Simba iliendelea kutawala mchezo na dakika ya 75 ikaongeza bao la tatu kupitia penalti iliyopigwa na Rushine de Reuck, baada ya Anthony Mligo kuangushwa ndani ya eneo la hatari.

Chama ahitimisha karamu ya mabao

Dakika ya 79, Clatous Chama alihitimisha ushindi huo kwa shuti kali nje ya boksi, akimalizia pasi safi kutoka kwa Suleiman Mwalimu. Bao hilo la nne liliihakikishia Simba ushindi mnono na tiketi ya fainali kwa kishindo.

Kwa ushindi huo mnono wa 4-0, Simba sasa inasubiri mshindi kati ya Azam FC na Yanga katika fainali ya CRDB Bank Cup. Mnyama ameonyesha wazi kuwa yuko katika ubora wa hali ya juu, na anawania kutwaa ubingwa kwa msimu huu kwa nguvu zote.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’