Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st June 2026


Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan

Ndoto za Tunisia katika Kombe la Dunia 2026 zimefikia tamati kwa njia ya kusikitisha baada ya kupokea kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa Japan katika mchezo wa Kundi F uliochezwa leo Jumapili Juni 21.

Matokeo hayo yameiacha Tunisia mkiani mwa kundi hilo huku ikipoteza mechi yake ya pili mfululizo, baada ya awali kufungwa mabao 5-1 na Sweden. Kipigo cha Japan kimeifanya timu hiyo kuruhusu mabao tisa katika mechi mbili, jambo linaloonyesha udhaifu mkubwa wa safu yao ya ulinzi.

Japan ilianza mchezo kwa kasi kubwa na kutawala umiliki wa mpira tangu dakika za mwanzo. Mashambulizi ya mara kwa mara yaliwalazimisha Watunisia kucheza muda mwingi katika eneo lao la hatari huku safu ya ulinzi ikionekana kuzidiwa na kasi na mbinu za wapinzani wao.

Daichi Kamada alifunga bao la kwanza dakika ya nne huku Ayase Ueda akifunga mabao mawili na Junya Ito akifunga bao la nne. Tunisia ilijaribu kujibu kupitia mipira ya kushtukiza lakini ilishindwa kuunda nafasi za kutosha za kuisumbua safu ya ulinzi ya Japan.

Kipigo hicho kinaifanya Japan kuimarisha nafasi yake ya kufuzu hatua ya 16 bora huku Tunisia ikibaki bila pointi yoyote baada ya michezo miwili.

Mashabiki wa Tunisia walionekana kuvunjika moyo baada ya kipenga cha mwisho huku wengi wakiamini timu yao haikuonyesha kiwango kinachostahili katika mashindano hayo makubwa. Kuaga kwa namna hii kunakuwa pigo kubwa kwa taifa hilo ambalo lilikuwa na matumaini ya kufanya vizuri zaidi katika michuano ya mwaka huu.

Tunisia hawakuwa wameruhusu bao lolote kwenye hatua ya kufuzu ambapo katika mechi 10, walishinda tisa na kutoka droo mchezo mmoja. Hata hivyo sasa wamepigwa mabao 9 kwenye mechi mbili tu


  

More Stories

Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Today, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Today, READ MORE β†’
Makocha Yanga, Azam FC watambiana kuelekea nusu fainali Kombe la CRDB
Makocha Yanga, Azam FC watambiana kuelekea nusu fainali Kombe la CRDB
Today, READ MORE β†’
Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Yesterday, READ MORE β†’
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Yesterday, READ MORE β†’