Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande

Joel JJ By Joel JJ • 21st June 2026


Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande

Liverpool FC inaendelea kuonyesha nia ya dhati kumsajili nyota chipukizi wa RB Leipzig RB Leipzig, Yan Diomande, baada ya ofa yao ya awali ya takribani €100 milioni kukataliwa na klabu hiyo ya Ujerumani.

Kwa mujibu wa taarifa,  Liverpool sasa inajiandaa kuwasilisha ofaa mpya iliyoboreshwa ili kuvunja pingamizi la Leipzig na kuingia hatua ya juu ya mazungumzo. 

Leipzig wagoma kumuuza Diomande

RB Leipzig imeendelea kusisitiza kuwa haina mpango wa kumuuza mchezaji huyo kwa sasa, ikipendelea kumbakiza kwa angalau msimu mmoja zaidi. Hata hivyo, inaripotiwa kuwa Diomande mwenyewe anaonyesha utayari wa kuondoka endapo makubaliano yatafikiwa kati ya vilabu. 

Klabu hiyo ya Bundesliga inaaminika kuweka thamani ya mchezaji huyo kati ya €100M hadi €120M+, kutokana na kiwango chake kilichopanda kwa kasi na mchango wake mkubwa ndani ya kikosi. 

PSG nao ndani ya kinyang’anyiro

Mbali na Liverpool, mabingwa wa Ufaransa Paris Saint-Germain (PSG) nao wanatajwa kuwa wanafuatilia kwa karibu mchakato wa uhamisho huo nyuma ya pazia.

Diomande kwa sasa yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Ivory Coast kinachoshiriki michuano ya kombe la Dunia inayoendelea Mexico, Canada na Marekani.


  

More Stories

Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Today, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Today, READ MORE →
Makocha Yanga, Azam FC watambiana kuelekea nusu fainali Kombe la CRDB
Makocha Yanga, Azam FC watambiana kuelekea nusu fainali Kombe la CRDB
Today, READ MORE →
Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Yesterday, READ MORE →
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Yesterday, READ MORE →