Liverpool FC inaendelea kuonyesha nia ya dhati kumsajili nyota chipukizi wa RB Leipzig RB Leipzig, Yan Diomande, baada ya ofa yao ya awali ya takribani €100 milioni kukataliwa na klabu hiyo ya Ujerumani.
Kwa mujibu wa taarifa, Liverpool sasa inajiandaa kuwasilisha ofaa mpya iliyoboreshwa ili kuvunja pingamizi la Leipzig na kuingia hatua ya juu ya mazungumzo.
Leipzig wagoma kumuuza Diomande
RB Leipzig imeendelea kusisitiza kuwa haina mpango wa kumuuza mchezaji huyo kwa sasa, ikipendelea kumbakiza kwa angalau msimu mmoja zaidi. Hata hivyo, inaripotiwa kuwa Diomande mwenyewe anaonyesha utayari wa kuondoka endapo makubaliano yatafikiwa kati ya vilabu.
Klabu hiyo ya Bundesliga inaaminika kuweka thamani ya mchezaji huyo kati ya €100M hadi €120M+, kutokana na kiwango chake kilichopanda kwa kasi na mchango wake mkubwa ndani ya kikosi.
PSG nao ndani ya kinyang’anyiro
Mbali na Liverpool, mabingwa wa Ufaransa Paris Saint-Germain (PSG) nao wanatajwa kuwa wanafuatilia kwa karibu mchakato wa uhamisho huo nyuma ya pazia.
Diomande kwa sasa yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Ivory Coast kinachoshiriki michuano ya kombe la Dunia inayoendelea Mexico, Canada na Marekani.



