Maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 yanaendelea kushika kasi jijini Arusha huku ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa ukiendelea kunoga siku hadi siku.
Muonekano wa uwanja huo unaonyesha hatua kubwa ya maendeleo, jambo linaloibua matumaini makubwa kwa Watanzania kuelekea mashindano hayo ya kihistoria Serikali kwa kushirikiana na wakandarasi imeendelea kusisitiza kuwa mradi huo unaenda sambamba na ratiba iliyopangwa, huku kazi mbalimbali za miundombinu ikiwemo maeneo ya watazamaji, vyumba vya wachezaji na huduma nyingine muhimu zikiendelea kutekelezwa kwa kasi.
Uwanja huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja bora vitakavyotumika katika AFCON 2027, mashindano ambayo Tanzania itakuwa mwenyeji kwa pamoja na nchi jirani za Kenya na Uganda. Kukamilika kwa mradi huu kunatarajiwa kuimarisha sekta ya michezo, kukuza utalii na kuacha alama ya kudumu katika maendeleo ya miundombinu ya michezo nchini.



