Baada ya Simba SC na Azam FC kufuzu fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank msimu wa 2025/26, mjadala mkubwa sasa umehamia kwenye uwanja utakaotumika kuchezwa pambano hilo la Julai 4, 2026.
Kwa misimu miwili mfululizo, fainali hiyo imefanyika Zanzibar katika dimba la New Amaan Complex, lakini safari hii wadau wengi wa soka wanaona ni wakati muafaka wa kuirejesha Dar es Salaam, jiji ambalo halijashuhudia fainali hiyo tangu msimu wa 2015/16.
Kutokana na maboresho yanayoendelea katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, viwanja vingine kama Uhuru Stadium na Azam Complex vinatajwa kuwa miongoni mwa chaguo zinazoweza kuandaa mchezo huo mkubwa unaotarajiwa kuvuta maelfu ya mashabiki.
Mikoa iliyowahi kuwa mwenyeji wa fainali ya Kombe la Shirikisho tangu 2015/16:
2015/16 β Dar es Salaam (Benjamin Mkapa)
2016/17 β Dodoma (Jamhuri Stadium)
2017/18 β Arusha (Sheikh Amri Abeid Stadium)
2018/19 β Lindi (Ilulu Stadium)
2019/20 β Rukwa (Nelson Mandela Stadium β Sumbawanga)
2020/21 β Kigoma (Lake Tanganyika Stadium)
2021/22 β Arusha (Sheikh Amri Abeid Stadium)
2022/23 β Tanga (Mkwakwani Stadium)
2023/24 β Zanzibar (New Amaan Complex)
2024/25 β Zanzibar (New Amaan Complex) Huku
TFF ikiwa bado haijatangaza rasmi venue ya fainali ya mwaka huu, macho na masikio ya mashabiki yameelekezwa kwenye uamuzi huo muhimu ambao utaamua mkoa gani utaandika historia nyingine ya mashindano hayo.



