Ligi Kuu ya NBC inaelekea ukingoni ambapo Jumanne ijayo, Juni 30 ligi hiyo itafikia tamati kwa mechi za mzunguuko wa 30 kupigwa.
Bodi ya ligi imethibitisha kuwa mechi zote za raundi ya 28, 29 na 30 zote zitapigwa muda mmoja saa 10 jioni. Lengo ni kuhakikisha hakuna uwezekano wa upangaji wa matokeo.
Wakati kukiwa na vita kali kwenye mbio za ubingwa kati ya Yanga na Simba, chini ya msimamo pia kuwa vita kali ambapo mkapa sasa KMC pekee wakiwa tayari wameteremka daraja.
Mbeya City iko nafasi ya 15 tofauti ya alama moja tu dhidi ya Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 14 na alama 26.
Kimahesabu kuanzia Dodoma Jiji inayoshika nafasi ya 8 na timu nyingine kushuka chini haziko salama.Β




