Alvarez aweka wazi mapenzi yake kwa Barcelona, Atletico yaweka ngumu kumuuza

Joel JJ By Joel JJ • 23rd June 2026


Alvarez aweka wazi mapenzi yake kwa Barcelona, Atletico yaweka ngumu kumuuza

Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Julián Álvarez, ameripotiwa kuongeza shinikizo la kutaka kuondoka Atlético Madrid ili kutimiza ndoto yake ya kujiunga na Barcelona, katika sakata linaloendelea kuvuta hisia kubwa kwenye soka la Ulaya.

Kwa mujibu wa taarifa, Álvarez ameonesha nia ya wazi ya kuangalia changamoto mpya ya kikazi, hali iliyoendelea kuibua maswali kuhusu hatma yake ndani ya klabu ya Atlético Madrid.

Barcelona ilituma ofa ya kwanza ya kumsajili nyota huyo wa Argentina inayokadiriwa kufikia euro 100M, lakini ikakataliwa kabla ya Real Madrid kuwasilisha ofa ya euro 150M ambayo nayo ilikataliwa.

Atlético Madrid wameweka msimamo mkali kuhusu mchezaji huyo, wakisisitiza kuwa hawana mpango wa kuuza kirahisi. Klabu hiyo inadaiwa kumwekea mkataba wa muda mrefu unaoendelea hadi 2030 pamoja na kipengele cha kuvunja mkataba kinachofikia takribani euro milioni 500.

Viongozi wa Atlético wanaamini kuwa Álvarez bado ni sehemu muhimu ya mipango yao ya muda mrefu, hivyo hawako tayari kupokea ofa isiyokidhi thamani ya mchezaji huyo.

Hata hivyo baada ya Alvarez mwenyewe kuweka hadharani matamanio yake ya kujiunga na Barcelona, hatua hiyo huenda ikafungua mlango mwingine wa majadiliano baina ya Barcelona na Atletico Madrid na pengine mwafaka kufikiwa siku za usoni.

Kwa sasa Alvarez yuko na kikosi cha Argentina kwenye michuano ya kombe la Dunia nchini Marekani.


  

More Stories

JS Kabylie Waachana na Ecua Celestine, Hatma yake na Yanga kujadiliwa
JS Kabylie Waachana na Ecua Celestine, Hatma yake na Yanga kujadiliwa
Today, READ MORE →
Ali Kamwe aahidi kumaliza hadithi za Azam FC Zanzibar
Ali Kamwe aahidi kumaliza hadithi za Azam FC Zanzibar
Today, READ MORE →
Mganga wa Ghana atishia kumlaani Mshambuliaji Harry Kane kabla ya mechi yao dhidi ya England
Mganga wa Ghana atishia kumlaani Mshambuliaji Harry Kane kabla ya mechi yao dhidi ya England
Today, READ MORE →
 Lumumba Vea Shabiki aliebadili dakika 90 kuwa Historia ,  Atua Marekani
Lumumba Vea Shabiki aliebadili dakika 90 kuwa Historia , Atua Marekani
Today, READ MORE →
Serengeti Girls yawinda taji la CECAFA dhidi ya Uganda
Serengeti Girls yawinda taji la CECAFA dhidi ya Uganda
Today, READ MORE →
Ahmed awatamani zaidi Yanga , Azam wagumu
Ahmed awatamani zaidi Yanga , Azam wagumu
Today, READ MORE →
Messi, Ronaldo wazidi kuwagawa mashabiki Duniani
Messi, Ronaldo wazidi kuwagawa mashabiki Duniani
Today, READ MORE →
Simba yawasili Morogoro tayari kuikabili Mtibwa Sugar
Simba yawasili Morogoro tayari kuikabili Mtibwa Sugar
Today, READ MORE →
Casemiro Aungana na Messi
Casemiro Aungana na Messi
Today, READ MORE →
Alvarez aweka wazi mapenzi yake kwa Barcelona, Atletico yaweka ngumu kumuuza
Alvarez aweka wazi mapenzi yake kwa Barcelona, Atletico yaweka ngumu kumuuza
Today, READ MORE →