Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 17, Serengeti Girls, leo itakuwa na kibarua kizito cha kuwania ubingwa wa #CECAFAU-17 dhidi ya Uganda katika mchezo wa fainali utakaopigwa kwenye dimba la #KMCComplex, Dar es Salaam.
Kikosi cha Tanzania kinachonolewa na Kocha msaidizi, Esther Chabruma kimefika fainali baada ya kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo, huku kikisaka kumalizia safari yake kwa kutwaa taji mbele ya mashabiki wa nyumbani.
Uganda nayo imeingia fainali ikiwa haijapoteza mchezo wowote, jambo linaloifanya mechi hiyo kutarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kati ya mataifa mawili yaliyokuwa katika kiwango bora tangu kuanza kwa mashindano.
Wakati huo huo, Kenya watakipiga dhidi ya South Sudan katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu, huku kila timu ikisaka kumaliza mashindano hayo kwa ushindi.



