Simba watamba kuvuna alama mbele ya Mtibwa Sugar, Barker akihitaji ushindi wa lazima

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media • 23rd June 2026


Simba watamba kuvuna alama mbele ya Mtibwa Sugar, Barker akihitaji ushindi wa lazima

Klabu ya Simba SC leo imekutana na waandishi wa habari katika mkutano rasmi kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar utakaochezwa kesho saa 10:00 jioni katika Uwanja wa Jamhuri. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku timu zote zikiwa na malengo muhimu katika hatua hii ya msimu.

Akizungumza na wanahabari, Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema maandalizi ya kikosi chake yamekamilika na wachezaji wako katika hali nzuri kuelekea pambano hilo. Barker amesisitiza kuwa lengo kubwa la timu yake ni kuhakikisha wanapata ushindi ili kuendelea kutimiza malengo waliyojiwekea msimu huu.

“Maandalizi kwa upande wetu yapo vizuri kuhakikisha tunashinda mchezo huu muhimu kwetu. Tunafahamu tunakwenda kucheza na timu inayopambana kujiweka katika mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi, hivyo tunatarajia mchezo mgumu lakini tuko tayari,” alisema Barker.

Kwa upande wake, beki wa Simba Nickson Kibabage amesema wachezaji wote wanaelewa uzito wa mchezo huo na umuhimu wa kupata alama tatu. Ameeleza kuwa kikosi kizima kimejipanga kufuata maelekezo ya benchi la ufundi ili kuhakikisha kinaondoka uwanjani na ushindi.

“Wachezaji wote tunafahamu umuhimu wa mchezo huu na tutaingia kwa umakini mkubwa kwa kufuata maelekezo ya benchi la ufundi ili kupata matokeo ya ushindi kama malengo yetu yalivyo,” amesema Kibabage.

Simba wanaingia katika mchezo huo wakihitaji kuendeleza matokeo mazuri huku Mtibwa Sugar nao wakisaka pointi muhimu za kuboresha nafasi yao kwenye msimamo wa ligi. Hivyo, mashabiki wanatarajia kushuhudia pambano kali na la kuvutia katika Uwanja wa Jamhuri kesho jioni.


  

More Stories

DARESSALAAMDERBY | “Sisi siyo timu ya kuweka vichwa chini...” – Ally Kamwe
DARESSALAAMDERBY | “Sisi siyo timu ya kuweka vichwa chini...” – Ally Kamwe
Today, READ MORE →
Maresca Mguu Sawa Man City
Maresca Mguu Sawa Man City
Today, READ MORE →
Je, tuwape heshima yao au wachukue kwa nguvu?
Je, tuwape heshima yao au wachukue kwa nguvu?
Today, READ MORE →
Simba watamba kuvuna alama mbele ya Mtibwa Sugar, Barker akihitaji ushindi wa lazima
Simba watamba kuvuna alama mbele ya Mtibwa Sugar, Barker akihitaji ushindi wa lazima
Today, READ MORE →
Yanga, Azam zatambiana kuelekea kesho
Yanga, Azam zatambiana kuelekea kesho
Today, READ MORE →
JS Kabylie Waachana na Ecua Celestine, Hatma yake na Yanga kujadiliwa
JS Kabylie Waachana na Ecua Celestine, Hatma yake na Yanga kujadiliwa
Today, READ MORE →
Ali Kamwe aahidi kumaliza hadithi za Azam FC Zanzibar
Ali Kamwe aahidi kumaliza hadithi za Azam FC Zanzibar
Today, READ MORE →
Mganga wa Ghana atishia kumlaani Mshambuliaji Harry Kane kabla ya mechi yao dhidi ya England
Mganga wa Ghana atishia kumlaani Mshambuliaji Harry Kane kabla ya mechi yao dhidi ya England
Today, READ MORE →
 Lumumba Vea Shabiki aliebadili dakika 90 kuwa Historia ,  Atua Marekani
Lumumba Vea Shabiki aliebadili dakika 90 kuwa Historia , Atua Marekani
Today, READ MORE →
Serengeti Girls yawinda taji la CECAFA dhidi ya Uganda
Serengeti Girls yawinda taji la CECAFA dhidi ya Uganda
Today, READ MORE →