Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe, amesema kikosi hicho kipo imara kiakili na kipo tayari kwa mchezo muhimu wa kesho wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Azam FC katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Kamwe amewataka wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kuendelea kuungana na timu katika michezo mitatu iliyosalia ya Ligi Kuu Tanzania Bara, akisisitiza kuwa nafasi ya kutwaa ubingwa wa tano mfululizo ni historia kubwa inayohitaji mshikamano, imani na sapoti kutoka kwa kila Mwananchi.
Aidha, amesema matokeo ya mchezo uliopita dhidi ya Azam FC hayawezi kuiondoa Yanga kwenye mstari wa mapambano ya ubingwa, kwani timu hiyo imeonyesha uimara mkubwa msimu mzima na bado ina nafasi kubwa ya kufikia malengo yake.
Kwa upande mwingine, Kamwe amesema mchezo huo si wa wachezaji pekee bali ni wa mashabiki pia, akiwahamasisha kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa New Amaan Complex ili kuisukuma timu kuelekea ushindi muhimu na hatua nyingine ya kuukaribia ubingwa wa ligi



