Timu ya Taifa ya Wanawake ya Burkina Faso, Les Étalons Dames, ipo katika kambi maalum ya Jeshi la SND Loumbila kwa mafunzo ya siku 10 yanayolenga kuimarisha uzalendo, nidhamu na mshikamano miongoni mwa wachezaji.
Mafunzo hayo yanafanyika chini ya uongozi wa kocha mkuu Pascal Sawadogo na benchi lake la ufundi, ikiwa ni sehemu ya mpango ulioanzishwa na Serikali ya Burkina Faso kwa timu zote za taifa kupitia Wizara ya Michezo.
Miongoni mwa wachezaji wanaoshiriki mafunzo hayo ni nyota wa Tausi FC, Judicaël Ouoba na Mounifatou Helbi, pamoja na mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo, Adama Congo. Mpango huo ulitangazwa mwezi Februari mwaka huu kwa lengo la kujenga uzalendo, kuongeza mshikamano na kuimarisha nidhamu kwa wanamichezo wanaowakilisha taifa lao



