Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ • 25th June 2026


Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu

Mabao mawili aliyofunga mshambuliaji wa Singida Black Stars Ndumumwe Mossi kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons jana yamemfanya afikishe mabao 14 sasa akimfikia Feisal Salum 'Fei Toto'.

Mossi aliyetua Singida BS kwenye usajili wa dirisha dogo, amekuwa shujaa wa Singida BS na kuifanya timu hiyo ijihakikishie ushiriki wa michuano ya kombe la Shirikisho (CAFCC) msimu ujao.

Wakati Mossi na Fei Toto wakichuana kileleni, Allan Okello (Yanga), Mathew Tegisi (Pamba Jiji) na Fabrice Ngoy (Namungo Fc) wanafuatia kila mmoja akiwa amefunga mabao 11.

Suleiman Mwalimu wa Simba yeye anaongoza kwa upande wa Wekundu hao wa Msimbazi akiwa amefunga mabao 9 akiwa sawa na nyota wa Yanga Prince Dube, Pacome Zouzoua na Mudathir Yahya.

Kuelekea mechi mbili za kuhitimisha msimu, ni wazi Fei Toto na Mossi wako katika nafasi nzuri zaidi ya kuibuka na tuzo hiyo.


  

More Stories

Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Today, READ MORE →
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Today, READ MORE →
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Today, READ MORE →
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Today, READ MORE →
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Today, READ MORE →
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Today, READ MORE →
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Today, READ MORE →
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Today, READ MORE →
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Today, READ MORE →
Neymar arejea Brazil ikitinga kibabe 32 bora kombe la Dunia
Neymar arejea Brazil ikitinga kibabe 32 bora kombe la Dunia
Today, READ MORE →