Mabao mawili aliyofunga mshambuliaji wa Singida Black Stars Ndumumwe Mossi kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons jana yamemfanya afikishe mabao 14 sasa akimfikia Feisal Salum 'Fei Toto'.
Mossi aliyetua Singida BS kwenye usajili wa dirisha dogo, amekuwa shujaa wa Singida BS na kuifanya timu hiyo ijihakikishie ushiriki wa michuano ya kombe la Shirikisho (CAFCC) msimu ujao.





