Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki

Joel JJ By Joel JJ • 25th June 2026


Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki

Klabu ya Yanga SC imeanza rasmi harakati za kumrejesha kiungo mshambuliaji wake wa zamani, Stephane Aziz Ki, kutoka klabu ya Al Ittihad, imefahamika.

Kwa mujibu wa taarifa, Yanga SC tayari imetuma ofa rasmi kwa Al Ittihad ikiwa ni sehemu ya mpango wa kumrudisha nyota huyo ambaye aliwahi kuwa MVP wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24 kabla ya kutimkia Morocco kujiunga na Wydad CA.

Aziz Ki kwa sasa yupo nchini kwa mapumziko baada ya kumaliza majukumu yake ya msimu nchini Libya, huku taarifa zikieleza kuwa mustakabali wake katika klabu hiyo ya Afrika Kaskazini bado hauko wazi.

Inaelezwa kuwa kiungo huyo raia wa Burkina Faso amekuwa na wasiwasi kuhusu mazingira ya kiusalama nchini Libya, jambo ambalo limechangia kufikiria uwezekano wa kurejea nchini, ambako aliwahi kufurahia mafanikio makubwa akiwa na Yanga SC.

Aidha, Aziz Ki anatajwa kutaka kuwa karibu zaidi na familia yake, hali inayoongeza uwezekano wa kuachana na Al Ittihad mapema kuliko ilivyotarajiwa.

Wakati Yanga SC ikiwa tayari imewasilisha ofa yake, bado mazungumzo kati ya klabu hizo mbili yanaendelea. Ikiwa makubaliano hayatofikiwa, inaelezwa kuwa mchezaji huyo anaweza kufungua shauri katika shirikisho la soka duniani FIFA akidai kutokamilika kwa baadhi ya malipo ya usajili kutoka kwa klabu yake ya sasa.

Kwa hali ilivyo, mashabiki wa Yanga SC wana kila sababu ya kuwa na matumaini, kwani uwezekano wa kumrejesha Aziz Ki Jangwani unaonekana kuwa mkubwa zaidi endapo mazungumzo yataenda vizuri.


  

More Stories

Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Today, READ MORE →
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Today, READ MORE →
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Today, READ MORE →
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Today, READ MORE →
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Today, READ MORE →
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Today, READ MORE →
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Today, READ MORE →
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Today, READ MORE →
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Today, READ MORE →
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Today, READ MORE →