Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika

Joel JJ By Joel JJ • 25th June 2026


Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika

Baada ya kukamilika kwa mechi za mzunguuko wa 28, unaweza kusema klabu za Yanga, Simba, Azam Fc na Singida BS tayari zimejihakikishia tiketi ya kushiriki mashindano ya CAF msimu ujao 2026/27.

Ushindi wa mabao 3-0 ambao Yanga waliupata dhidi ya Azam Fc umewafanya wafikishe alama 69 ambazo ni Simba pekee inayoweza kuzifikia katika mechi zilizobaki.

Nao Wekundu wa Msimbazi baada ya kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0, wamefikisha alama 67 ambazo hakuna timu nyingine zilizochini yake inayoweza kuzifikia.

Hivyo ni rasmi vigogo hao wa soka nchini msimu ujao wataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya ligi ya mabingwa (CAFCL).

Vita iliyopo baina yao katika mechi mbili zilizobaki ni kuamua nani anakwenda kuwa bingwa Yanga wakiwa na faida ya alama 2 mkononi.

Licha ya kupigo cha mabao 3-0 dhidi ya Yanga, klabu ya Azam Fc imejihakikishia kumaliza nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakikusanya alama 58.

Hakuna timu chini yake ambayo inaweza kufikia idadi hiyo ya alama. Faida kama hiyo pia wanayo Singida BS ambao jana waliichapa Tanzania Prisons mabao 3-1 na kufikisha alama 50. 

Vita kali bado iko chini ya msimamo ambapo timu 6 ziko hatarini kushuka daraja au kucheza play-off. Tanzania Prisons wanashika nafasi ya 15 wakiwa na alama 26 wakati Mashujaa Fc wanashika nafasi ya 10 wakiwa na alama 30.


  

More Stories

Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Today, READ MORE →
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Today, READ MORE →
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Today, READ MORE →
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Today, READ MORE →
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Today, READ MORE →
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Today, READ MORE →
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Today, READ MORE →
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Today, READ MORE →
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Today, READ MORE →
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Today, READ MORE →