Baada ya kukamilika kwa mechi za mzunguuko wa 28, unaweza kusema klabu za Yanga, Simba, Azam Fc na Singida BS tayari zimejihakikishia tiketi ya kushiriki mashindano ya CAF msimu ujao 2026/27.
Ushindi wa mabao 3-0 ambao Yanga waliupata dhidi ya Azam Fc umewafanya wafikishe alama 69 ambazo ni Simba pekee inayoweza kuzifikia katika mechi zilizobaki.
Nao Wekundu wa Msimbazi baada ya kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0, wamefikisha alama 67 ambazo hakuna timu nyingine zilizochini yake inayoweza kuzifikia.
Hivyo ni rasmi vigogo hao wa soka nchini msimu ujao wataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya ligi ya mabingwa (CAFCL).
Vita iliyopo baina yao katika mechi mbili zilizobaki ni kuamua nani anakwenda kuwa bingwa Yanga wakiwa na faida ya alama 2 mkononi.
Licha ya kupigo cha mabao 3-0 dhidi ya Yanga, klabu ya Azam Fc imejihakikishia kumaliza nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakikusanya alama 58.
Hakuna timu chini yake ambayo inaweza kufikia idadi hiyo ya alama. Faida kama hiyo pia wanayo Singida BS ambao jana waliichapa Tanzania Prisons mabao 3-1 na kufikisha alama 50.
Vita kali bado iko chini ya msimamo ambapo timu 6 ziko hatarini kushuka daraja au kucheza play-off. Tanzania Prisons wanashika nafasi ya 15 wakiwa na alama 26 wakati Mashujaa Fc wanashika nafasi ya 10 wakiwa na alama 30.




