Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu • 25th June 2026


Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?

Kaimu Afisa Habari wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Yahya Abushehe, amesema siku chache zilizobaki za NBC Premier League zitakuwa na majibu ya maswali mengi yanayowasumbua mashabiki wa soka nchini, ikiwemo nani atatwaa ubingwa, nani atasalia ligi kuu na nani atashuka daraja.

Abushehe ametoa kauli hiyo baada ya kupongeza namna mechi zote nane za mzunguko uliopita zilivyochezwa kwa wakati mmoja na kuoneshwa mubashara kupitia Azam TV, jambo alilosema limeongeza ushindani na kuwapa mashabiki fursa ya kufuatilia kila kinachoendelea katika mbio za ubingwa na vita ya kushuka daraja.

Ameeleza kuwa macho ya wengi sasa yataelekezwa kwenye michezo ya Juni 27 na Juni 30, ambapo hatima ya msimu wa 2025/26 itaamuliwa. Swali kubwa likiwa ni kama bingwa atapatikana mapema Juni 27 au kama ushindani utaendelea hadi mchezo wa mwisho wa msimu.

Mbali na mbio za ubingwa, Abushehe amesema vita ya kusalia ligi kuu nayo imezidi kupamba moto huku baadhi ya timu zikihitaji matokeo mazuri ili kuepuka kushuka daraja au kucheza mechi za mtoano.

"Majibu yote yatapatikana katika siku hizi za mwisho za msimu. Mashabiki waendelee kufuatilia kwa sababu kila mchezo una umuhimu mkubwa," amesema Abushehe.

Kwa sasa, mashabiki wa soka Tanzania wanasubiri kwa hamu kuona nani atakayetwaa taji la NBC Premier League na ni timu zipi zitakazofanikiwa kutimiza malengo yao kabla ya pazia la msimu kushushwa rasmi.


  

More Stories

Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Bingwa atajulikana Juni 27 au hadi mwisho wa msimu?
Today, READ MORE →
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Nne bora ya mashindano ya CAF 2026/27 imekamilika
Today, READ MORE →
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Cr 7, Thierry Henry, Ibrahimovic Waingia kwenye Mjadala mzito wa Soka Mtandaoni
Today, READ MORE →
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Hadithi ya Kushangaza ya Eric Roy na Brest
Today, READ MORE →
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Msigwa; Mashindano Mengi ni Ufunguo Wa Kuinua Vipaji Vya Soka
Today, READ MORE →
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Martin Dúbravka kutua Tottenham Hotspurs, Vicario aweka nia ya kuondoka.
Today, READ MORE →
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Yanga yatuma ofa Al Ittihad, kumrejesha Aziz Ki
Today, READ MORE →
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Ally Kamwe, Tupo pamoja na Azam
Today, READ MORE →
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Mossi akoleza moto mbio za ufungaji bora Ligi Kuu
Today, READ MORE →
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Morocco yaendeleza ubabe kombe la Dunia, yaifumua Haiti 4-2 na kutinga 32 bora
Today, READ MORE →