Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Simba SC dhidi yaSingida BS utapigwa katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, uliopo jijini Dar es Salaam.
Mchezo huo wa raundi ya 29 umepangwa kuchezwa Jumamosi saa 10 jioni, kama ilivyo kwa michezo mingine yote ya raundi hiyo ambayo pia itaanza kwa wakati mmoja.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, michezo yote ya raundi ya 29 itachezwa saa 10 jioni, huku timu zote zikipaswa kucheza mechi zao za raundi ya 29.
Uwanja wa KMC Complex utatumika kwa mchezo kati ya Yanga SC na TRA United, hali iliyosababisha Simba SC kurejea tena kucheza katika uwanja wa Isamuhyo kwa sababu JKT Tanzania watakuwa ugenini mkoani Mwanza dhidi ya Pamba Jiji.
Simba na Singida BS ni mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na umuhimu wake katika hatua za mwisho za msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Ni mchezo ambao Simba inahitaji ushindi ili kuendelea kusalia kwenye mbio za ubingwa kwani kama watakosa ushindi na Yanga kushinda mchezo dhidi ya TRA United, ni wazi ubingwa utaelekea Jangwani mapema kwa msimu wa tano mfululizo



