Kocha Mkuu wa Singida BS, Muhimu Kanu, amesema kikosi chake kinaingia kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Simba SC kikiwa na lengo la kushinda, akisisitiza kuwa timu inayotaka kuiwakilisha Tanzania kimataifa inapaswa kuwa na uwezo wa kuifunga Simba. Kanu alitoa kauli hiyo Juni 26, 2026, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa NBC Premier League utakaopigwa Juni 27.





