Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th June 2026


Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS

Kiungo mkabaji na nahodha wa timu ya taifa ya Uganda, Khalid Aucho, anatajwa kuwa kwenye mazungumzo na klabu ya Singida Black Stars kuhusu kusitisha mkataba wake, licha ya mkataba huo kutarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu wa 2026/27.

Taarifa kutoka chanzo cha uhakika imebainisha kuwa pande zote mbili zimeanza majadiliano ya kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba huo kwa maridhiano.

Aucho alijiunga na Singida Black Stars msimu uliopita akitokea Yanga SC, baada ya kumaliza kipindi cha mafanikio cha misimu mitatu akiwa Jangwani. Hata hivyo, maisha yake ndani ya Singida BS hayajawa rahisi.

Kiungo huyo amekumbwa na majeraha ya mara kwa mara yaliyomfanya kukosa mechi nyingi za timu yake. Mbali na changamoto za majeraha, aliwahi pia kusimamishwa na klabu kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu kabla ya kurejeshwa kikosini.

Katika kipindi chake akiwa Yanga, Aucho alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu waliochangia mafanikio makubwa ya klabu hiyo katika mashindano ya ndani na kimataifa, kiwango kilichomfanya kuwa miongoni mwa viungo bora katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Tetesi zimedokeza kuwa Aucho huenda akarejea klabu yake ya zamani Gor Mahia ya Kenya


  

More Stories

Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Today, READ MORE β†’
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Today, READ MORE β†’
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Today, READ MORE β†’
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Today, READ MORE β†’
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
Today, READ MORE β†’
Senegal waandika historia kombe la Dunia, huku wakiishikilia hatma yao mkononi
Senegal waandika historia kombe la Dunia, huku wakiishikilia hatma yao mkononi
Today, READ MORE β†’
Pigo kubwa kwa England, Reece James nje kwa angalau wiki Mbili
Pigo kubwa kwa England, Reece James nje kwa angalau wiki Mbili
Today, READ MORE β†’
Lumumba kivutio Kombe la Dunia licha ya matokeo mabaya ya DR Congo
Lumumba kivutio Kombe la Dunia licha ya matokeo mabaya ya DR Congo
Yesterday, READ MORE β†’
Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS
Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS
Yesterday, READ MORE β†’
Valverde na wenzake wamgeukia Bielsa, Mvutano Wazidi kambi ya Uruguay.
Valverde na wenzake wamgeukia Bielsa, Mvutano Wazidi kambi ya Uruguay.
Yesterday, READ MORE β†’