Local,Transfer News,Tetesi, Singida, Gor Mahia, Yanga

Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 Jun 2026
Aucho kwenye mazungumzo ya kusitisha mkataba na Singida BS

Kiungo mkabaji na nahodha wa timu ya taifa ya Uganda, Khalid Aucho, anatajwa kuwa kwenye mazungumzo na klabu ya Singida Black Stars kuhusu kusitisha mkataba wake, licha ya mkataba huo kutarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu wa 2026/27.

Taarifa kutoka chanzo cha uhakika imebainisha kuwa pande zote mbili zimeanza majadiliano ya kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba huo kwa maridhiano.

Aucho alijiunga na Singida Black Stars msimu uliopita akitokea Yanga SC, baada ya kumaliza kipindi cha mafanikio cha misimu mitatu akiwa Jangwani. Hata hivyo, maisha yake ndani ya Singida BS hayajawa rahisi.

Kiungo huyo amekumbwa na majeraha ya mara kwa mara yaliyomfanya kukosa mechi nyingi za timu yake. Mbali na changamoto za majeraha, aliwahi pia kusimamishwa na klabu kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu kabla ya kurejeshwa kikosini.

Katika kipindi chake akiwa Yanga, Aucho alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu waliochangia mafanikio makubwa ya klabu hiyo katika mashindano ya ndani na kimataifa, kiwango kilichomfanya kuwa miongoni mwa viungo bora katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Tetesi zimedokeza kuwa Aucho huenda akarejea klabu yake ya zamani Gor Mahia ya Kenya

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’