Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th June 2026


Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia

Timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) imeandika historia mpya baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Uzbekistan na kufuzu kwa mara ya kwanza hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026.

DR Congo ilijikuta nyuma mapema kufuatia bao la Uzbekistan, lakini ilionyesha moyo wa kupambana na kurejea kwa nguvu katika kipindi cha pili. Yoane Wissa alisawazisha kwa mkwaju wa penalti kabla ya mshambuliaji Fiston Mayele kufunga bao la pili lililowapa Leopards uongozi na kuamsha shangwe kubwa kwa mashabiki wao.

Wissa alikamilisha ushindi huo kwa kufunga bao la tatu dakika za nyongeza.

Kwa Mayele, hili lilikuwa bao lake la kwanza katika fainali za Kombe la Dunia, akiendelea kuthibitisha ubora wake kwenye jukwaa kubwa zaidi la soka duniani.

Ushindi huo umeiwezesha DR Congo kutinga hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza katika historia yake ya ushiriki wa Kombe la Dunia, ikiwa ni miaka 52 tangu iliposhiriki kwa mara ya mwisho mwaka 1974 ikiwa inajulikana kama Zaire. Katika hatua ya 32 bora, DR Congo itavaana na England katika pambano litakalokuwa na ushindani mkubwa.

Historia imeandikwa, na sasa macho ya Waafrika wengi yataelekezwa kwa Leopards wakisaka kuendelea kufanya maajabu kwenye Kombe la Dunia 2026.

Hatua ya 32 bora DR Congo watachuana na Uingereza


  

More Stories

Hatua ya Makundi  Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa,  32 Bora Kuanza Leo
Hatua ya Makundi Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa, 32 Bora Kuanza Leo
Today, READ MORE β†’
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Today, READ MORE β†’
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Today, READ MORE β†’
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Today, READ MORE β†’
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Today, READ MORE β†’
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Yesterday, READ MORE β†’
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Yesterday, READ MORE β†’
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Yesterday, READ MORE β†’
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
Yesterday, READ MORE β†’