International,Normal News,World Cup, Congo, Local

Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jun 2026
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia

Timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) imeandika historia mpya baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Uzbekistan na kufuzu kwa mara ya kwanza hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026.

DR Congo ilijikuta nyuma mapema kufuatia bao la Uzbekistan, lakini ilionyesha moyo wa kupambana na kurejea kwa nguvu katika kipindi cha pili. Yoane Wissa alisawazisha kwa mkwaju wa penalti kabla ya mshambuliaji Fiston Mayele kufunga bao la pili lililowapa Leopards uongozi na kuamsha shangwe kubwa kwa mashabiki wao.

Wissa alikamilisha ushindi huo kwa kufunga bao la tatu dakika za nyongeza.

Kwa Mayele, hili lilikuwa bao lake la kwanza katika fainali za Kombe la Dunia, akiendelea kuthibitisha ubora wake kwenye jukwaa kubwa zaidi la soka duniani.

Ushindi huo umeiwezesha DR Congo kutinga hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza katika historia yake ya ushiriki wa Kombe la Dunia, ikiwa ni miaka 52 tangu iliposhiriki kwa mara ya mwisho mwaka 1974 ikiwa inajulikana kama Zaire. Katika hatua ya 32 bora, DR Congo itavaana na England katika pambano litakalokuwa na ushindani mkubwa.

Historia imeandikwa, na sasa macho ya Waafrika wengi yataelekezwa kwa Leopards wakisaka kuendelea kufanya maajabu kwenye Kombe la Dunia 2026.

Hatua ya 32 bora DR Congo watachuana na Uingereza

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
7h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
13h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
19h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’