Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th June 2026


Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama

Timu ya Taifa ya Uingereza imeonyesha ubora wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Panama katika mchezo wa mwisho wa Kundi L na kutinga hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026 ikiwa kinara wa kundi.

Baada ya kipindi cha kwanza kumalizika bila mabao, Uingereza ilirejea kwa kasi kipindi cha pili ambapo Jude Bellingham alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 62 kwa shuti kali lililoivunja ngome ya Panama. Dakika tano baadaye, nahodha Harry Kane alifunga bao la pili kwa kichwa akimalizia pasi ya Bellingham na kuhitimisha ushindi muhimu wa Three Lions.

Bao hilo lilikuwa la 11 kwa Kane katika historia ya Kombe la Dunia, likimfanya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Uingereza katika michuano hiyo baada ya kumpita Gary Lineker. Wakati huo huo, Bellingham aliendelea kung'ara kwa kufunga bao moja na kutoa asisti moja katika mechi hiyo.

Ushindi huo umeifanya Uingereza kumaliza kileleni mwa Kundi L ikiwa na pointi saba, ikifuatiwa na Croatia, huku Ghana ikifuzu kama moja ya timu bora zilizomaliza nafasi ya tatu. Panama ilimaliza mkiani mwa kundi na kuaga mashindano bila kufuzu hatua ya mtoano.

Katika hatua ya 32 bora, Uingereza itakutana na DR Congo, timu iliyomaliza nafasi ya pili katika Kundi K baada ya ushindi wake wa mabao 3-1 dhidi ya Uzbekistan. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku England ikisaka kuendeleza safari yake ya kutwaa taji la dunia kwa mara ya pili katika historia yake.


  

More Stories

Hatua ya Makundi  Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa,  32 Bora Kuanza Leo
Hatua ya Makundi Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa, 32 Bora Kuanza Leo
Today, READ MORE β†’
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Today, READ MORE β†’
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Today, READ MORE β†’
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Today, READ MORE β†’
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Today, READ MORE β†’
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Yesterday, READ MORE β†’
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Kante afanana na Che Malone? makosa madogo yanayoweza kumgharimu Simba
Yesterday, READ MORE β†’
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Cape Verde Gumzo la Dunia, Kutoka kuwa wageni hadi 32 bora WC2026
Yesterday, READ MORE β†’
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
France yatinga 32 Bora kombe la dunia kibabe ikiichapa Norway, Dembele akiweka rekodi
Yesterday, READ MORE β†’