Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 29th June 2026


Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe

Uongozi wa Yanga SC umekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa klabu hiyo ipo katika mazungumzo ya kumuajiri kocha Fadlu Davids, ukisisitiza kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanyika kuhusu suala hilo.

Kupitia afisa habari wa klabu hiyo Ally Kamwe, ameeleza kuwa taarifa hizo si za kweli na hazitokani na uongozi wa klabu. Uongozi huo umebainisha kuwa ongezeko la uvumi huo linachangiwa na hamu ya kutaka kupata taarifa za haraka kuhusu mipango ya klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya twiga na jangwani , hali inayowapa nafasi baadhi ya watu kusambaza taarifa zisizo na uthibitisho.

Klabu hiyo imewataka wanachama na mashabiki wake kuendelea kupata taarifa kupitia vyanzo rasmi pekee, ikieleza kuwa taarifa zote zinazohusu usajili wa wachezaji, mabadiliko ya benchi la ufundi na masuala mengine ya klabu zitatolewa kupitia YANGA APP pamoja na kurasa rasmi za Yanga SC kwenye mitandao ya kijamii.

Aidha, uongozi wa Yanga umefafanua kuwa taarifa yoyote kuhusu usajili wa kocha au mchezaji inayotolewa nje ya vyanzo hivyo rasmi inapaswa kupuuzwa hadi pale klabu itakapotoa tamko rasmi.

Wakati huo huo, Yanga imewataka mashabiki wake kuelekeza nguvu na umoja wao katika mchezo ujao wa NBC Premier League, ikiwahimiza kujitokeza kwa wingi uwanjani kuisapoti timu katika harakati za kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu.


  

More Stories

Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe
Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe
Today, READ MORE β†’
Brazil wapindua meza kibabe, Na kuiondoa Japan kombe la dunia 2026
Brazil wapindua meza kibabe, Na kuiondoa Japan kombe la dunia 2026
Today, READ MORE β†’
Kocha wa zamani Yanga aibukia Tunisia
Kocha wa zamani Yanga aibukia Tunisia
Today, READ MORE β†’
Fei Toto, Mossi, Okello watatoana damu ufungaji bora
Fei Toto, Mossi, Okello watatoana damu ufungaji bora
Today, READ MORE β†’
Enzo atambulishwa Man City, ataweza kuziba pengo la Guardiola?
Enzo atambulishwa Man City, ataweza kuziba pengo la Guardiola?
Today, READ MORE β†’
Moalin - Tunahitaji Ushindi Tuwe Mabingwa
Moalin - Tunahitaji Ushindi Tuwe Mabingwa
Today, READ MORE β†’
Mechi tatu kupigwa leo ndani ya kombe la dunia 2026, Hatua ya 32 Bora.
Mechi tatu kupigwa leo ndani ya kombe la dunia 2026, Hatua ya 32 Bora.
Today, READ MORE β†’
Moallin au Steve Barker, dakika 90 za mwisho za kuandika historia ya ubingwa
Moallin au Steve Barker, dakika 90 za mwisho za kuandika historia ya ubingwa
Today, READ MORE β†’
Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao
Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao
Today, READ MORE β†’
Pamba Jiji Yakabiliwa Na Hatari Ya Kuporomoka Kikosi, Nyota Wake Wahusishwa Na Timu Mbalimbali
Pamba Jiji Yakabiliwa Na Hatari Ya Kuporomoka Kikosi, Nyota Wake Wahusishwa Na Timu Mbalimbali
Today, READ MORE β†’