Ndoto za Ujerumani kutwaa Kombe la Dunia 2026 zimefikia tamati baada ya Paraguay kuibuka na ushindi wa kihistoria wa mikwaju ya penalti kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 za mchezo wa hatua ya mtoano uliochezwa kwenye Uwanja wa Boston Stadium. Ushindi huo umeifanya Paraguay kuandika moja ya matokeo makubwa zaidi ya kushtua katika mashindano ya mwaka huu na kufuzu hatua inayofuata.
Paraguay walionekana wenye kujiamini tangu mwanzo wa mchezo na kufanikiwa kupata bao la uongozi kabla ya ujerumani kurejesha bao ilo kupitia mshambuliaji wa taifa ilo na timu ya arsenal K.Havert na kufanya mchezo kuelekea dakika 30 za ziada.
Baada ya dakika 120 kumalizika bila kupatikana mshindi, mchezo ukamuliwa kwa mikwaju ya penalti. Hapo ndipo Paraguay walipoonyesha utuulivu mkubwa, huku Ujerumani ikigharamiwa na makosa ya Kai Havertz, Nick Woltemade na Jonathan Tah waliokosa penalti zao. JosΓ© Canale aliifungia Paraguay penalti ya ushindi na kuamsha shangwe kubwa kwa mashabiki wa taifa hilo.
Ushindi huo unaingia kwenye historia ya soka la Paraguay ukiwa ni mara ya pili kwa taifa hilo kushinda mchezo wa Kombe la Dunia kupitia mikwaju ya penalti. Pia ni moja ya matokeo makubwa ya kushtua katika hatua za mtoano, ikizingatiwa Paraguay inaingia mashindanoni ikiwa nafasi ya 41 katika viwango vya FIFA, huku Ujerumani ikiwa nafasi ya 10 duniani.
Kwa Ujerumani, matokeo hayo yanaongeza kipindi kigumu ambacho taifa hilo limekuwa likikipitia kwenye Kombe la Dunia. Baada ya kutolewa katika hatua ya makundi mwaka 2018 na 2022, safari yao ya mwaka 2026 imefikia mwisho mapema tena, hali inayozidi kuongeza presha kwa timu hiyo kurejea kwenye ubora wake wa zamani.
Paraguay sasa inaelekeza macho yake katika hatua inayofuata ya mashindano ikiwa na ari kubwa baada ya kuiondoa moja ya mataifa yenye historia kubwa zaidi katika soka la dunia. Ushindi huo si tu umeipeleka mbele Paraguay, bali pia umeonyesha kwamba katika Kombe la Dunia 2026 hakuna timu inayoweza kupewa ushindi kabla ya filimbi ya mwisho.



