Mshambuliaji wa Singida BS Ndumumwe Mossi amefunga hat-trik yake ya pili msimu huu licha ya klabu yake kukubali kipigo cha mabao 4-3 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa mwisho uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Mossi ameibuka kuwa mfungaji bora baada ya kufikisha mabao 17 akimpiku Feisal Salum 'Fei Toto' wa Azam Fc ambao licha ya kuongoza mbio hizo kwa muda mrefu, amemaliza msimu na mabao 15.
Nafasi ya tatu imeenda kwa Allain Okello ambaye ameweka kambani mabao 14.




