Uongozi wa JKT Tanzania umetoa salamu za pole na kuomba radhi kufuatia jeraha alilopata kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua, katika mchezo wa mwisho wa msimu wa 2025/26 wa NBC Premier League uliochezwa Juni 30, 2026 kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.
Kupitia taarifa rasmi, uongozi wa JKT Tanzania umesema umeguswa na tukio hilo na umeomba radhi kwa niaba ya mchezaji wao, Hassan Wahabi, ambaye alihusika katika tukio lililosababisha Pacome kuumia wakati wakipambana kuwania mpira.
Klabu hiyo imemtakia Pacome nafuu ya haraka na kurejea uwanjani akiwa katika afya njema, ikisisitiza kuwa tukio hilo halikuwa la makusudi bali lilitokea katika harakati za kawaida za mchezo wa soka.



