Vita ya ufungaji bora kombe la dunia 2026 imeendelea kushika baada ya apo jana Nahodha na mshambuliaji wa ufaransa Klyian Mbappe kupachika kambani mabao mawili katika ushindi wa mabao matatu wa taifa lake dhidi ya Sweden kwenye mchezo wa 32 bora.
Mabao hayo yanamfanya Nahodha huyu wa ufaransa kufikisha jumla ya mabao sita akilingaana na mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi ambae pia amekwisha weka kambani mabao sita kwenye michezo mitatu ya hatua ya makundi .
Mbali na vita ya ufungaji bora kwa mashindano ya kombe la dunia 2026 Pia mabao hayo yanamfanya mbappe ambaye anashiriki kwa mara ya tatu michuano ya kombe la dunia kufikisha mabao 18 huku akiwa nyuma kwa bao moja pekee nyuma ya Lionel Messi ambaye ndie kinara katika historia ya wafungaji bora muda wote wa kombe la dunia akiwa na mabao 19.



