Timu ya Kinondoni Municipal Council KMC imeshukuru mashabiki wake kutokana na mapenzi makubwa walionyesha licha ya wakati mgumu ndani ya timu hiyo uliopelekea kushuka daraja msimu wa 2025-26 .
Ligi hiyo ambayo imetamatika apo jana , KMC imemaliza msimu ikiwa nafasi ya mwisho 16 ikikusanya alama 9 pekee huku ikifunga magoli 16 na kuruhusu mabao 53 , ligi hiyo inayojumlisha michezo 30 kwa kila timu KMC ilifanikiwa kushinda michezo miwili pekee , sare tatu na kupoteza michezo 25 .
KMC itashiriki championship msimu wa 2026-27 huku mategemeo yao ni kurejea ligi kuu msimu wa 2027-28




