Mlinzi raia wa Ivory Coast Chamou Karaboue ametangaza rasmi kung'atuka ndani ya kikosi Cha Simba sports club kufuatia kutamatika kwa mkataba wake na miamba hiyo ya msimbazi.
Taarifa hiyo imetolewa na mchezaji huyo kupitia mtandao wake rasmi wa kijamii huku akiwashukuru wachezaji wenzake , viongozi na mashabiki wa Timu hiyo.
" Baada ya miaka miwili muda umefika wakusema Asante , asanteni kwa kila kitu naondoka katika Timu hii lakini sehemu ya mimi itabaki apa " amesema Chamou.
Karaboue alijiunga na Simba msimu wa 2023-24 na kutumikia msimu mmoja pekee kabla ya kutolewa kwa mkopo TRA United ambayo ameitukia msimu wa huu wa 2025-26



