Uzinduzi wa kampeni ubingwa wa Yanga sc msimu wa 2025-26 umefanyika hii leo makao makuu ya club hiyo , ambapo uzinduzi huo umelenga mambo mbalimbali yenye kulenga namna timu hiyo imepanga kusherekea ubingwa huo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Afisa habari na mawasiliano wa timu hiyo Ally Kamwe ameeleza wamejipanga vilivyo kufanya sherehe hizo huku slogan ya sherehe hizo ikiitwa " Mwakani Tena " ikilenga kuwajibu wanaolalamikia ubingwa wa timu hiyo .
Yanga sc imetwaa ubingwa huo apo jana baada ya kumaliza msimu ikiwa na alama 75 mbili zaidi ya watani zao simba waliomaliza nafasi ya pili , Yanga katika msimu wa 2025-26 kwenye michezo 30 ya NBC ilifanikiwa kushinda michezo 23 , sare 6 na kupoteza mchezo mmoja pekee .



