Dube aiweka Yanga njia panda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd July 2026


Dube aiweka Yanga njia panda

Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, wanakabiliwa na uamuzi mgumu kuhusu hatma ya mshambuliaji wao tegemeo, Prince Dube, baada ya mkataba wake kumalizika huku akitajwa kuwa kwenye rada za klabu kadhaa ndani na nje ya Afrika.

Taarifa kutoka vyanzo vya ndani ya uongozi wa Yanga zinaeleza kuwa nyota huyo wa Zimbabwe amewaomba viongozi wa klabu hiyo wamruhusu kutafuta changamoto mpya nje ya Tanzania, akiamini ni wakati sahihi wa kupiga hatua nyingine katika maisha yake ya soka baada ya kuitumikia Yanga kwa mafanikio makubwa kwa misimu miwili.

Chanzo hicho kimebainisha kuwa Dube tayari amepokea ofa kutoka klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, huku pia akihusishwa na klabu za nchini kwao Zimbabwe ambazo ni Hardrock FC na Scottland FC.Β 

Licha ya msimamo wa Dube kutaka kujaribu soka la nje, Yanga bado haijakata tamaa. Viongozi wa mabingwa hao wanaendelea na jitihada za kumshawishi nyota huyo kuongeza mkataba na kubaki Jangwani, wakiamini bado ana nafasi kubwa katika mipango ya benchi la ufundi kuelekea msimu mpya.

Awali kulikuwa na taarifa kwamba Yanga na Dube walikuwa kwenye mazungumzo ya kuongeza mkataba wake, huku pande zote zikionekana kukaribia makubaliano. Hata hivyo, taarifa za sasa kutoka ndani ya klabu zinaonyesha kuwa mshambuliaji huyo ameonyesha nia ya kutafuta changamoto mpya nje ya Tanzania.

Katika msimu uliomalizika, Dube alifunga mabao 10 na kubaki kuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa Yanga. Mbali na uwezo wake wa kucheza kama mshambuliaji wa kati, pia ameonyesha ubora akiwa anacheza kutokea pembeni, jambo lililomfanya kuwa silaha muhimu katika safu ya ushambuliaji.

Katika mechi za mwisho za msimu dhidi ya Azam FC na JKT Tanzania, Dube alicheza zaidi akitokea pembeni, ambapo alitoa mchango mkubwa kwa kufunga na kutengeneza mabao

Pia amekuwa na kiwango kizuri akiwa na timu ya taifa ya Zimbabwe, hali iliyochangia kuongezeka kwa idadi ya klabu zinazomfuatilia kuelekea dirisha hili la usajili.


  

More Stories

Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Today, READ MORE β†’
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Today, READ MORE β†’
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Today, READ MORE β†’
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Today, READ MORE β†’
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Today, READ MORE β†’
Dube aiweka Yanga njia panda
Dube aiweka Yanga njia panda
Today, READ MORE β†’
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Today, READ MORE β†’
England yaiondoa DR Congo kombe la dunia 2026, Harry kane akiendelea kuonyesha makali
England yaiondoa DR Congo kombe la dunia 2026, Harry kane akiendelea kuonyesha makali
Today, READ MORE β†’
Barcelona kuzindua Uzi wao mpya utakaotumika msimu ujao.
Barcelona kuzindua Uzi wao mpya utakaotumika msimu ujao.
Today, READ MORE β†’
Laporta athibitisha, Barcelona imetuma ofa Atletico kumsajili Alvarez
Laporta athibitisha, Barcelona imetuma ofa Atletico kumsajili Alvarez
Today, READ MORE β†’