Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd July 2026


Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch

Klabu ya Simba SC imefikia hatua za mwisho za kumsajili kiungo wa kimataifa wa Nigeria Ibraheem Jabaar kutoka Stellenbosch FC ya Afrika Kusini.

Taarifa zinaeleza kuwa makubaliano ya awali kati ya Simba SC na mchezaji huyo yamekamilika na anatarajiwa kuwasili Tanzania kwa ajili ya kukamilisha usajili wake rasmi.

Vyanzo kutoka ndani ya uongozi wa Simba, vimedokeza kuwa Jabaar ameandaliwa mkataba wa miaka miwili ambao utamuweka katika klabu hiyo hadi mwaka 2028 iwapo kila kitu kitakwenda kama ilivyopangwa.

Usajili huu umefanyika kufuatia mapendekezo ya kocha Steve Barker ambaye anafahamu vyema uwezo wa mchezaji huyo kutokana na kufanya naye kazi hapo awali.

Barker anaamini Jabaar anaweza kuongeza ubora katika safu ya kiungo ya Simba kuelekea msimu wa 2026/27 kutokana na uelewa wake wa mfumo wa uchezaji.

Jabaar mwenye umri wa miaka 23 ameondoka Stellenbosch akiwa mchezaji huru baada ya kushindwa kufikia makubaliano ya mkataba mpya. Akiwa klabuni hapo amecheza zaidi ya mechi 140, akifunga mabao sita na kutoa pasi saba za mabao.

Ana uwezo wa kucheza kama kiungo wa kati, kiungo mshambuliaji na winga wa kushoto, hali inayompa kocha chaguo zaidi katika safu ya ushambuliaji.


  

More Stories

Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Today, READ MORE β†’
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Today, READ MORE β†’
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Today, READ MORE β†’
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Today, READ MORE β†’
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Today, READ MORE β†’
Dube aiweka Yanga njia panda
Dube aiweka Yanga njia panda
Today, READ MORE β†’
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Today, READ MORE β†’
England yaiondoa DR Congo kombe la dunia 2026, Harry kane akiendelea kuonyesha makali
England yaiondoa DR Congo kombe la dunia 2026, Harry kane akiendelea kuonyesha makali
Today, READ MORE β†’
Barcelona kuzindua Uzi wao mpya utakaotumika msimu ujao.
Barcelona kuzindua Uzi wao mpya utakaotumika msimu ujao.
Today, READ MORE β†’
Laporta athibitisha, Barcelona imetuma ofa Atletico kumsajili Alvarez
Laporta athibitisha, Barcelona imetuma ofa Atletico kumsajili Alvarez
Today, READ MORE β†’