Aliyekuwa Mkurugenzi wa Yanga , Paul Matthews, hii Leo amejiunga na klabu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini ambako atahudumu kama Sporting Director kuelekea msimu wa 2026/27.
Matthews anaondoka Yanga baada ya kuhudumu kwa msimu mmoja, akisimamia masuala ya kiufundi ya klabu ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati ya maendeleo ya timu, kuboresha muundo wa idara ya soka na kushirikiana na benchi la ufundi katika kuendeleza kiwango cha kikosi cha kwanza pamoja na vipaji vya vijana.
Kabla ya kujiunga na Yanga mwaka 2025, Matthews alifanya kazi kwa zaidi ya muongo mmoja katika SuperSport United, ambako alijijengea sifa katika eneo la usajili na ukuzaji wa vipaji. Pia aliwahi kufanya kazi katika klabu za AmaTuks, Jomo Cosmos na Tembisa Classic, akikusanya uzoefu mkubwa katika maendeleo ya wachezaji na uchambuzi wa kiufundi.
Marumo Gallants wanamteua Matthews ikiwa ni sehemu ya mabadiliko makubwa ya kiutawala na kiufundi kuelekea msimu mpya, wakiamini uzoefu wake utasaidia kuimarisha mfumo wa uendeshaji wa klabu na kuongeza ushindani wao katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini



