Yanga yapata pigo lingine

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 2nd July 2026


Yanga yapata pigo lingine

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Yanga , Paul Matthews, hii Leo amejiunga na klabu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini ambako atahudumu kama Sporting Director kuelekea msimu wa 2026/27.

Matthews anaondoka Yanga baada ya kuhudumu kwa msimu mmoja, akisimamia masuala ya kiufundi ya klabu ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati ya maendeleo ya timu, kuboresha muundo wa idara ya soka na kushirikiana na benchi la ufundi katika kuendeleza kiwango cha kikosi cha kwanza pamoja na vipaji vya vijana.

Kabla ya kujiunga na Yanga mwaka 2025, Matthews alifanya kazi kwa zaidi ya muongo mmoja katika SuperSport United, ambako alijijengea sifa katika eneo la usajili na ukuzaji wa vipaji. Pia aliwahi kufanya kazi katika klabu za AmaTuks, Jomo Cosmos na Tembisa Classic, akikusanya uzoefu mkubwa katika maendeleo ya wachezaji na uchambuzi wa kiufundi.

Marumo Gallants wanamteua Matthews ikiwa ni sehemu ya mabadiliko makubwa ya kiutawala na kiufundi kuelekea msimu mpya, wakiamini uzoefu wake utasaidia kuimarisha mfumo wa uendeshaji wa klabu na kuongeza ushindani wao katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini


  

More Stories

Spain wafanikiwa kutinga Hatua ya 16 Bora WC26 Kibabe.
Spain wafanikiwa kutinga Hatua ya 16 Bora WC26 Kibabe.
Today, READ MORE β†’
Yanga yapata pigo lingine
Yanga yapata pigo lingine
Today, READ MORE β†’
Dube Aikacha Yanga na Kurejea Kwao Zimbabwe
Dube Aikacha Yanga na Kurejea Kwao Zimbabwe
Today, READ MORE β†’
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Today, READ MORE β†’
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Tonali na Mateus Fernandez watua Spurs
Today, READ MORE β†’
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Kichapo dhidi ya Ubelgiji , Kiungo Matata Senegal Atoa Nyongo kwa Benchi lake la Ufundi
Today, READ MORE β†’
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Ahmed Ally aongeza miaka miwili JKT Tanzania
Today, READ MORE β†’
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Simba mbioni kumalizana na kiungo mahiri Stellenbosch
Today, READ MORE β†’
Dube aiweka Yanga njia panda
Dube aiweka Yanga njia panda
Today, READ MORE β†’
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Ubelgiji wapindua meza kibabe kwa mara nyingine, Wakiwaondoa Senegal WC26
Today, READ MORE β†’