Kikosi Cha wekundu wa msimbazi Simba hii leo kimeondoka jijini Dar es salaam kuelekea visiwani Zanzibar ikiwa ni siku Moja kabla ya mchezo wa fainali dhidi ya Azam fc unaotarajiwa kufanyika mjini Pemba apo kesho.
Simba imeondoka ikiwa na kikosi chake kamili kuelekea mchezo huo utakaochezwa majira ya saa 11 za jioni katika uwanja wa Gombani , ambao utahodhi kwa mara ya kwanza mtanange wa Mzizima derby.
Simba inaelekea mchezo huu ikiwa na hari kubwa itokanayo na kukosa Taji la ligi wikiendi iliyopita mbele ya watani zao Yanga , huku wapinzani wao Azam FC wanaingia kwenye mchezo huu Wakiwa na matumaini pekee ya kutwaa Taji katika msimu wa 2025-26 , kufuatia kukosa mataji yote walioshiriki msimu huu .




