Ahmed Ali atamba: Tukitwaa Kombe la CRDB, tutafanya paredi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd July 2026


Ahmed Ali atamba: Tukitwaa Kombe la CRDB, tutafanya paredi

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ali, amesema klabu hiyo ipo tayari kuandika historia nyingine kwa kutwaa Kombe la CRDB, akisisitiza kuwa iwapo wataibuka mabingwa, kutakuwa na sherehe kubwa na paredi litakaloendana na hadhi ya klabu hiyo.

Akizungumza wakati kikosi hicho kikielekea Pemba kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa fainali dhidi ya Azam FC utakaopigwa Uwanja wa Gombani, Ahmed alisema taji la CRDB lina thamani kubwa kwa Simba na mashabiki wake, hivyo ushindi utastahili kusherehekewa kwa kiwango cha juu.

"Niweke wazi tu, kama tunachukua kombe hili tutasherehekea. Tutafanya sherehe kulingana na hadhi na ukubwa wa klabu yetu pamoja na ukubwa wa kombe lenyewe."

Ahmed aliongeza kuwa sherehe hizo hazitakuwa za kawaida, bali zitakuwa na mpangilio maalumu unaoendana na hadhi ya Simba.

"Litakuwa ni paredi lenye hadhi ya nyota tano na siyo mchaka mchaka."

Simba yajiamini kabla ya Fainali

Licha ya kukiri kuwa Azam FC ni mpinzani mwenye ubora na anayetakiwa kuheshimiwa, Ahmed amesema Simba inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na imani kubwa ya kuibuka na ushindi.

Amesisitiza kuwa kikosi hicho kina ubora wa kutosha na kinafahamu uzito wa mchezo huo kwa mashabiki wa klabu hiyo.

"Ni fainali, mpinzani wetu tunajua ubora na ugumu wake, lakini ni wazi sisi ni bora na wakubwa zaidi yake. Tuna uhitaji mkubwa wa kombe hili, watu waliotutuma ni wengi kuliko waliowatuma wao."

Ahmed amesema nguvu kubwa ya Simba kuelekea mchezo huo inatokana na mashabiki wake, ambao wameendelea kuipa timu morali na hamasa ya kupambana hadi dakika ya mwisho.

"Sisi tuna sauti nyingi nyuma yetu ambazo zinatusukuma tuwapelekee kombe hili. Mashabiki wetu wanatupa mzuka, morali na ari ya kupambana kuelekea mchezo huu wa fainali."

Amehitimisha kwa kusisitiza kuwa dhamira ya Simba ni moja tu, kuibuka mabingwa wa CRDB Cup na kuwarejeshea furaha mashabiki wao baada ya msimu wenye changamoto.

"Tuko hapa tukiwa na dhamira moja tu, kuchukua Kombe la CRDB na kuwapelekea mashabiki wetu."

Fainali hiyo kati ya Simba na Azam FC inatarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi wa soka nchini, huku Simba ikisaka ubingwa wake wa nne wa CRDB Cup na kuendeleza rekodi yake ya kutopoteza fainali yoyote tangu mashindano hayo yaliporejea mwaka 2015.


  

More Stories

Jumba la maajabu laiponza Yanga, yatozwa faini Tsh Milioni 100
Jumba la maajabu laiponza Yanga, yatozwa faini Tsh Milioni 100
Today, READ MORE β†’
Kinda Fountain Gate mbioni kutua KRC Genk
Kinda Fountain Gate mbioni kutua KRC Genk
Today, READ MORE β†’
Djigui Diarra amaliza msimu akiwa mfalme wa clean sheets
Djigui Diarra amaliza msimu akiwa mfalme wa clean sheets
Today, READ MORE β†’
Azam Fc yamnasa winga hatari Sc Villa
Azam Fc yamnasa winga hatari Sc Villa
Today, READ MORE β†’
Ahmed Ali atamba: Tukitwaa Kombe la CRDB, tutafanya paredi
Ahmed Ali atamba: Tukitwaa Kombe la CRDB, tutafanya paredi
Today, READ MORE β†’
Madrid wavunja ukimya kuhusu tetesi za kumsajili kiungo wa Chelsea, Enzo fernandez.
Madrid wavunja ukimya kuhusu tetesi za kumsajili kiungo wa Chelsea, Enzo fernandez.
Today, READ MORE β†’
Man United waingia kwenye mazungumzo na winga wa West Ham, wakiendelea kupush kwa Baleba pia.
Man United waingia kwenye mazungumzo na winga wa West Ham, wakiendelea kupush kwa Baleba pia.
Today, READ MORE β†’
Simba waifuata Azam kibabe
Simba waifuata Azam kibabe
Today, READ MORE β†’
Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia
Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia
Today, READ MORE β†’
Ureno yaokoka kwa chupuchupu, yatinga16 bora baada ya kuitoa Croatia 2-1
Ureno yaokoka kwa chupuchupu, yatinga16 bora baada ya kuitoa Croatia 2-1
Today, READ MORE β†’