Simba Sc ni mabingwa wapya wa CRDB FEDERATION CUP baada ya kuiduiza Azam FC bao kwa Nunge katika mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Gombani mjini Pemba .
Simba imeshinda ubingwa huo baada ya bao la kujifunga la kiungo Yahya Zaid uliotokana na mpira wa kufa uliochongwa na winga hatari wa Simba Libasaa Gueye.
Mara ya mwisho kwa Simba kutwaa ubingwa wa FA ni msimu wa 2020-21 ambapo ilipata ubingwa huo mbele ya watani zao Yanga , pia huu unakuwa ubingwa wa pili kwa Simba msimu huu 2025-26 baada ya kushinda Taji la Muungano.
Katika mchezo huu pia ulizalisha kadi nyekundu kwa kiungo mshambuliaji wa Azam FC , Feisal Salumu kufuatia kumpiga kwa makusudi winga Libbasa Gueye.



