Haina kupoa, Brazil kukutana uso kwa uso na Norway kwenye fainali ya wc26

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media • 5th July 2026


Haina kupoa, Brazil kukutana uso kwa uso na Norway kwenye fainali ya wc26

Macho ya dunia yataelekezwa kwenye pambano kubwa la hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia 2026, ambapo Brazil watamenyana na Norway usiku wa leo kuanzia saa 5:00 usiku (23:00 EAT). Timu zote zinaingia uwanjani zikiwa na lengo moja tu – kushinda na kutinga robo fainali.

Brazil, mabingwa mara tano wa dunia, wanaendelea na ndoto ya kutwaa taji lao la sita. Baada ya kuiondoa Japan kwa ushindi wa mabao 2-1 katika hatua iliyopita, Seleção wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa na morali kubwa na wakiamini uzoefu wao unaweza kuwavusha tena.

Kwa upande wa Norway, kikosi hicho kinaendelea kuwa miongoni mwa timu zilizovutia zaidi katika mashindano haya. Wakiongozwa na mshambuliaji hatari Erling Haaland, waliinyoa Côte d’Ivoire mabao 2-1 na sasa wanaamini wana uwezo wa kuandika historia kwa kuwaondoa vigogo wa soka duniani.

Pambano hili pia linatarajiwa kuwa vita ya nyota, huku Haaland akitarajiwa kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Norway, wakati Brazil wakimtegemea ubora wa kikosi chao chenye uzoefu na wachezaji wenye uwezo wa kubadili matokeo kwa muda mfupi.

Mshindi wa mchezo huu atafuzu hatua ya robo fainali na kuendelea kusaka ndoto ya ubingwa wa dunia, huku timu itakayopoteza ikimaliza rasmi safari yake katika Kombe la Dunia 2026.


  

More Stories

Haina kupoa, Brazil kukutana uso kwa uso na Norway kwenye fainali ya wc26
Haina kupoa, Brazil kukutana uso kwa uso na Norway kwenye fainali ya wc26
Today, READ MORE →
Jamal Bakhresa ailalamikia bodi ya ligi na TFF kuhusu Azam fc
Jamal Bakhresa ailalamikia bodi ya ligi na TFF kuhusu Azam fc
Today, READ MORE →
France wafuzu robo fainali kombe la dunia 2026, Rasmi kukutana na Morroco
France wafuzu robo fainali kombe la dunia 2026, Rasmi kukutana na Morroco
Today, READ MORE →
Morroco wafuzu Robo fainali kombe la dunia 2026, Akiwaondoa wenyeji Canada
Morroco wafuzu Robo fainali kombe la dunia 2026, Akiwaondoa wenyeji Canada
Today, READ MORE →
MAGORI : Hizi ndiyo njia zetu , Ligi zikiwa za haki
MAGORI : Hizi ndiyo njia zetu , Ligi zikiwa za haki
Today, READ MORE →
Mtazamo wako ni upi kufuatia kadi nyekundu ya Feisal Salumu
Mtazamo wako ni upi kufuatia kadi nyekundu ya Feisal Salumu
Today, READ MORE →
Tukutane Kesho Airport , Paredi Ipo : Ahmed Ally
Tukutane Kesho Airport , Paredi Ipo : Ahmed Ally
Today, READ MORE →
Simba mabingwa CRDB FEDERATION CUP , Azam wakijinyonga Wenyewe
Simba mabingwa CRDB FEDERATION CUP , Azam wakijinyonga Wenyewe
Today, READ MORE →
Pilato fainali ya Simba na Azam Hadharani
Pilato fainali ya Simba na Azam Hadharani
Yesterday, READ MORE →
Barker na Ibenge wakutana kimya, vita uwanjani leo
Barker na Ibenge wakutana kimya, vita uwanjani leo
Yesterday, READ MORE →