Timu ya Mbeya city imeibuka na ushindi katika mchezo wa mkondo wa kwanza ( playoffs ) baada ya kuinyuka Tanzania Prison jumla ya mabao mawili kwa sifuri.
Katika mchezo huo uliochezwa katika Dimba la sokoine mkoani Mbeya , mabao ya Mbeya city yamewekwa kimiana na Noushad kabla ya msumari wa pili kuwekwa kimiani dakika za mwisho wa mchezo na Hijjah Shamte.
Ushindi huo unafanya Mbeya city kutanguliza Mguu mmoja kurejee ligi kuu bara , ambapo watasuburi matokeo ya mchezo wa marejeano utakaochezwa jumatano ya Julia 8 mwaka huu .
Mshindi wa jumla baina ya timu hizi atakata tiketi kushiriki ligi kuu bara msimu wa 2026-27 huku atayepoteza atacheza playoff nyingine dhidi ya mshindi wa playoff ya championship



