Azam FC imekamilisha usajili wa winga wa Ivory Coast, Kipre Jr (26), kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu wa mashindano wa 2026/27.
Kipre Jr anarejea Chamazi kwa mara nyingine baada ya kupita misimu miwili tangu alipoondoka Azam FC na kujiunga na klabu ya MC Alger ya Algeria.
Kwa mujibu wa makubaliano ya usajili huo, MC Alger imekubali kumuuza mchezaji huyo kwa Azam FC huku ikiweka kipengele kitakachowapa asilimia 30 ya ada ya uhamisho endapo Azam FC watamuuza Kipre Jr kwenda klabu nyingine siku zijazo.



