Nyota wa Yanga, Kibwana Shomari, amefichua kuwa jambo la kwanza alilofanya baada ya kupokea mshahara wake wa kwanza akiwa Mtibwa Sugar ni kumnunulia mama yake nyumba.
Shomari amesema Mama yake hakuwa na makazi yake binafsi na alikuwa akiishi kwa ndugu, hali iliyompa msukumo mkubwa wa kubadilisha maisha yake mara tu alipoanza kupata kipato kupitia soka la kulipwa.
"Nilipopokea mshahara wangu wa kwanza nikiwa Mtibwa Sugar, nilimnunulia mama yangu nyumba. Hakuwa na sehemu yake ya kuishi, alikuwa anaishi kwa ndugu," amesema Shomari.
Simulizi hiyo ya kugusa hisia inaonyesha namna ambavyo wachezaji wengi hutumia mafanikio yao kurejesha fadhila kwa familia zao, hususan wazazi waliowalea na kuwaunga mkono katika safari yao ya kufikia mafanikio.



