Kama mipango ya klabu ya Simba SC haitabadilika, basi timu hiyo inaweza kutumia michuano ya CECAFA Kagame Cup kama sehemu ya maandalizi ya msimu mpya (pre-season), kutokana na ratiba kubana na kutokuwepo kwa muda wa mapumziko marefu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Simba SC, Crencentius Magori, amesema klabu inahitaji kuhakikisha maandalizi ya msimu ujao yanaanza mapema, hususan kwa kusajili wachezaji wapya mapema ili kumsaidia kocha Steve Barker kujenga muunganiko imara wa kikosi kabla ya mashindano ya CAF kuanza.
Magori amesema baada ya mapumziko mafupi na kuongeza wachezaji wachache katika maeneo muhimu, Simba itachanganya maandalizi ya msimu ujao na michuano ya Kagame Cup ili kujiweka sawa kwa msimu wa 2026/27.
Amesema: βTutacombine maandalizi ya msimu ujao (pre-season) pamoja na CECAFA Kagame Cup ili kujiandaa na mashindano ya 2026/27.β



