Mpango wa Yanga kumpata Fadlu Davids wagonga mwamba

Joel JJ By Joel JJ • 6th July 2026


Mpango wa Yanga kumpata Fadlu Davids wagonga mwamba

Uongozi wa Yanga SC umeendelea na mchakato wa kusaka kocha mkuu mpya atakayechukua nafasi iliyoachwa na Pedro Gonçalves, lakini mipango ya awali ya kumleta kocha Fadlu Davids imekumbwa na changamoto na hatimaye mazungumzo kuvunjika.

Awali, mabingwa hao wa Tanzania Bara walikuwa kwenye mazungumzo ya karibu na Fadlu Davids, ambaye aliwahi kuzinoa klabu za Raja Casablanca ya Morocco na Simba ya Tanzania, kwa lengo la kumkabidhi jukumu la kuongoza kikosi hicho kuelekea msimu ujao wa mashindano ya ndani na kimataifa.

Sababu za kuvunjika mazungumzo

Kwa mujibu wa mwandishi na mchambuzi wa soka kutoka Afrika Kusini, Ayabonga Mthembu, pande zote mbili zimeshindwa kufikia makubaliano kutokana na tofauti kwenye masuala ya kifedha, hususan mfumo wa malipo na bonasi za mafanikio.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mazungumzo yalikuwa yamefikia hatua nzuri kabla ya kukwama katika vipengele vya mwisho vya mkataba, hali iliyosababisha Yanga kuhitimisha mazungumzo hayo kwa muda huo.

Baada ya dili hilo kugonga mwamba, Yanga sasa inaendelea na mchakato wa kumtafuta kocha mpya ambaye atakamilisha mradi uliowekwa na uongozi wa klabu hiyo.

Inaripotiwa kuwa huenda jina la kocha huyo mpya likafahamika ndani ya siku chache zijazo, pengine kabla ya mwisho wa wiki hii, huku uongozi ukiendelea kufanya tathmini ya wagombea waliobaki kwenye orodha fupi.

Hatma ya benchi la muda bado haijajulikana

Aidha, Yanga bado haijatoa tamko rasmi kuhusu hatma ya benchi la ufundi la muda lililoongozwa na makocha Abdihamid Moallin na Patrick Mabedi.

Makocha hao waliiongoza Yanga katika michezo saba ya mwisho wa msimu, ambapo walipoteza mechi mbili moja dhidi ya Dodoma Jiji kwenye Ligi Kuu na nyingine dhidi ya Azam FC katika nusu fainali ya Kombe la CRDB.

Hata hivyo, licha ya matokeo hayo, waliweza kufanikisha lengo kuu la msimu kwa kuisaidia Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya tano mfululizo.


  

More Stories

Neymar aaga Brazil kwa huzuni kubwa
Neymar aaga Brazil kwa huzuni kubwa
Today, READ MORE →
Spurs yamtambulisha Sandro Tonali katika usajili wa rekodi
Spurs yamtambulisha Sandro Tonali katika usajili wa rekodi
Today, READ MORE →
Mpango wa Yanga kumpata Fadlu Davids wagonga mwamba
Mpango wa Yanga kumpata Fadlu Davids wagonga mwamba
Today, READ MORE →
Rais Samia Suluhu Hassan amtembelea Pacome Hospitalini leo
Rais Samia Suluhu Hassan amtembelea Pacome Hospitalini leo
Today, READ MORE →
Simba Sc yaweza kutumia Kagame Cup kama pre-season Magori atoa maelezo
Simba Sc yaweza kutumia Kagame Cup kama pre-season Magori atoa maelezo
Today, READ MORE →
Mshahara wangu wa kwanza nlimjengea Mama nyumba - Kibwana
Mshahara wangu wa kwanza nlimjengea Mama nyumba - Kibwana
Today, READ MORE →
Azam FC wamrejesha Kipre Jr kutoka MC Alger
Azam FC wamrejesha Kipre Jr kutoka MC Alger
Today, READ MORE →
Steve Barker: mwakani nataka paredi kubwa zaidi na makombe yote ikiwezekana
Steve Barker: mwakani nataka paredi kubwa zaidi na makombe yote ikiwezekana
Today, READ MORE →
Pablo Franco Martinez aandika historia Morocco, MAS Fez watwaa ubingwa baada ya miaka 41
Pablo Franco Martinez aandika historia Morocco, MAS Fez watwaa ubingwa baada ya miaka 41
Today, READ MORE →
England yaiondoa Mexico Kombe la Dunia, sasa kuvaana na Norway robo fainali
England yaiondoa Mexico Kombe la Dunia, sasa kuvaana na Norway robo fainali
Today, READ MORE →